31.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Omog ataka mbili za majaribio kabla ya Yanga

Kocha Mkuu wa Azam FC, Joseph Omog
Kocha Mkuu wa Azam FC, Joseph Omog

NA ZAITUNI KIBWANA

KOCHA Mkuu wa Azam FC, Joseph Omog, ametaka mechi mbili za majaribio kabla ya timu yake haijapambana na Yanga kwenye mechi ya Ngao ya Jamii.

Azam na Yanga zinatarajia kukutana Septemba 13, katika Uwanja wa Taifa kwenye mechi hiyo, inayoashiria kuanza kwa msimu mpya wa ligi.

Omog ambaye kwa sasa amerudi Dar es Salaam, baada ya kuondolewa kwenye michuano ya Kombe la Kagame alisema mechi hizo zitamsaidia kukiweka sawa kikosi chake.

“Alisema timu yake imepata uzoefu katika michuano ya Kombe la Kagame, ila anataka mechi nyingine mbili kwa ajili ya kujiweka sawa,” alisema.

Alisema kikosi chake kitaanza mazoezi rasmi kuanzia leo, baada ya mapumziko aliyotoa kwa wachezaji wake mara baada ya kurejea Dar es Salaam.

“Mechi hizo siwezi kusema nataka kucheza na nani, ila nataka timu yoyote itakayoweza kukipima kikosi changu kabla ya mechi yetu na Yanga,” alisema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles