31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Mmoja wa pacha waliotenganishwa afariki dunia

Aveline Kitomary, Dar es Salaam

Mmoja wa pacha waliotenganishwa nchini Saudi Arabia na kurejea nchini Agosti 30, mwaka huu, Anisia Bernard, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Septemba 3.

Daktari aliyekuwa akiwahudumia watoto hao, Dk. Petronila Ngiloi amesema chanzo cha pacha huyo kupoteza maisha ni baada ya kutapika kwa muda mrefu na matatizo kwenye utumbo hali iliyosababisha kupoteza maji mengi na kushindwa kula chakula.

“Tangu walivyotoka safarini mmoja alionekana hakuwa na hali nzuri na tulivyotoka uwanja wa ndege tulikwenda moja kwa moja hospitali kumfanyia uchunguzi baada ya kuanza kutapika na kupandisha homa, hali hiyo iliyosababisha ashindwe hata kula lakini tukiwa kwenye ndege alikuwa anatapika.

“Hata hivyo vipimo ulioonesha kulikuwa na hitilafu kwenye utumbo ulikuwa umejikunja tulimfanyia upasuaji lakini hali iliendelea kuwa mbaya na baadaye kupoteza maisha akiwa ICU,” amesema Dk. Ngiloi.

Pacha hao Anisia na Melnes, walizaliwa January 29, mwaka jana wakiwa wameungana huko Misenyi mkoani Kagera na kupelekwa nchini Saudi Arabia kwa ajili ya kutenganishwa kazi iliyofanikiwa na kurudishwa nchini Agosti 31, mwaka huu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles