24.3 C
Dar es Salaam
Monday, September 16, 2024

Contact us: [email protected]

Mitaala 79 shahada ya uzamili yapitiwa upya

Na Esther Mnyika, Mtanzania Digital

JUMLA ya mitaala 79 ya shahada ya uzamili imepitiwa upya, huku 22  ikianzishwa katika shahada za awali  na uzamili kupitia  mradi wa HEET.

Hayo  yamesemwa  na Kaimu Mkurugenzi wa Elimu ya Juu kutoka  Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk. Kenneth Hosea wakati akifungua  mkutano   wadau  mbalimbali ambao utudumu kwa siku  mbili  leo Novemba 6,2023 jijini  Dar es Salaam.

Wadau  hao wamekutana kujadili  na kutoa mapendekezo ya  kuboresha mapitio ya mitaala  ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) na kutoa  maoni  ya uanzishwaji wa kampasi ya chuo  hicho mkoani Kigoma.

Dk. Hosea   amesema anatambua kuwa kama nchi wana changamoto na uhaba mkubwa ya rasilimali watu wenye ujuzi na ubora kwenye sekta ya  afya.

Amesema lengo  mojawapo  la mradi wa HEET  hapo MUHAS ni kupitia upya mitaala ya uzamili na kubuni mipya  kulingana na mahitaji ya nchi.

‘Jumla ya mitaala 16 ya shahada za uzamili imeanzishwa ambapo mitaala mitatu imeshapata ithibati  kutoka Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU) na inaanza kutumika mwaka huu na mitaala  ya 13 itajadiliwa kwenye  mkutano huu,”ameeleza.

Amesema mabadiliko ya elimu ya juu  yanayolenga taasisi maalum kama MUHAS yanahitaji  ushirikiano mpana na makini wa wadau ili kuhakikisha kwa mapitio ya mitaala yanashughulikia changamoto kubwa za rasilimali watu.

Amesema  shughuli hizo mbili zipo ndani ya maeneo nane ya mradi wa elimu  ya juu kwa  mabadiliko ya uchumi (HEET) ambao ni mageuzi ya elimu ya juu kwa maendeleo ya uchumi hususani katika sekta ya afya.

” Siku hii ni muhimu  yenye  maan kubwa  kufungua  mkutano  huu muhimu  wa wadau ili kujadili mapitio ya mitaala katika jitihada  za kuleta mabadiliko  ya elimu  yetu ya juu kwaajili  ya kuleta mageuzi  ya kiuchumi nchini, “amesema Dk. Hosea.

Naye Naibu Makamu Mkuu wa MUHAS, Profesa Apolinary Kamuhabwa, amesema  mwaka huu wanaadhimisha miaka 60 tangu kuanzishwa chuo hicho  wakiwa na  lengo la  kuongeza idadi ya watumishi wa afya.

“Ushiriki wa wadau ni sehemu  muhimu  ya mitaala ya elimu ya juu, kwa ushiriki  huu tunahakikisha matokeo ya mafunzo na ujuzi ambao wanafunzi  wamepata unawiana na mahitaji ya sasa na ya baadaye ya waajiri na jamii,” amesema Profesa Kamuhabwa.

Aidha amesema  kwa  kuhusisha wadau  hawa katika mapitio ya mitaala taasisi za elimu ya  juu zinaweza kuongeza  umuhimu na ushawishi program zao na kutayarisha wahitimu wao kwa changamoto na fursa za karne ya 21 mbeleni.

Naye Naibu wa Mradi wa HEET MUHAS, Dk. Nathanael Sirili, amesema kupata maoni ya wadau  ni muhimu hivyo  ujenzi wa kampasi  ya  Ujiji  mkoni Kigoma unatarajia kuanza mwakani na utachukua muda wa miezi 24 hadi kukamilka.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles