25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Majuto: Kuhiji kunanipa wakati mgumu wa kuigiza

majuto (2)NA THERESIA GASPER

MSANII nguli wa vichekesho nchini, Amri Athumani ‘King Majuto’, amesema anapata shida na aina ya uigizaji kwa sasa baada ya kwenda kuhiji na kuwa Alhaji.

Akizungumza jana katika Ofisi za New Habari, King Majuto, alisema   unapokwenda kuhiji unatakiwa kufuata sheria za dini na mambo yenye hekima na kujiepusha na vitu ambavyo havitakiwi kwenye dini.

“Vitu hivi vinakuwa ni vigumu  kuviepuka na hasa katika kazi zetu kwani unakuta unaigiza na mtu kama mke wako na sisi sheria zetu haziruhusu kuwa naye karibu hiyo ni moja ya changamoto kubwa ambayo naikwepa,” alisema Majuto.

Hata hivyo, mchekeshaji huyo alisema kuwa anatimiza ahadi zote za dini yake na kujitahidi kuepuka vitu ambavyo havitakiwi japokuwa ni vigumu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles