30.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

KOREA KUSINI YAITAKA MAREKANI KUSITISHA MAZOEZI YA KIJESHI

SEOUL, KOREA KUSINI


RAIS wa Korea Kusini, Moon Jae-In, ameitaka Marekani kusitisha kwa muda mazoezi yake ya kijeshi nchini hapa ili kupisha michuano ya Olimpiki itakayofanyika mapema mwakani.

Amesema hii itasaidia pia kuifanya Korea Kaskazini kutokuwa na shaka juu ya uwepo wa wanamichezo wake kwenye michuano hiyo.

Korea Kusini ni mwenyeji wa michezo hiyo itakayofanyika kwenye mji wa Pyeongchang Februari, kilomita 80 kutoka mpaka wake na Korea Kaskazini.

Mapema Canada na Marekani ziliapa kuendeleza mazoezi hayo ili kuishinikiza Korea Kaskazini kuachana na mpango wake wa nyuklia.

Michuano ya Olimpiki ya majira ya baridi inatarajiwa kuhusisha pia wanamichezo kutoka Korea Kaskazini jambo ambalo Rais Jae-In anaeleza ni fursa ya kuimarisha uhusiano zaidi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles