25.8 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

Jokate: Wasanii wa kike niungeni mkono

Jokate-Mwegelo-KidotiNA VICTORIA PATRICK (TSJ)

MWANAMITINDO, Joketi Mwegelo ‘Kidoti’, amewataka wasanii wenzake hasa wa kike wamtie nguvu kwa kununua bidhaa zake badala ya maneno matupu.

Mrembo huyo ambaye ni Miss Tanzania namba mbili mwaka 2006, alifafanua kwamba wasanii wengi wa kike wamekuwa wakisifia bidhaa zake kwa maneno lakini hawamuungi mkono kwa kuzinunua.

Jokate ambaye pia ni mwanamuziki na mwigizaji, alisema wasanii hao wakitumia bidhaa zake zitamuongezea kipato na kumtangaza yeye pamoja na taifa kwa ujumla kwa kuwa wasanii hao wana majina makubwa ndani na nje ya nchi.

“Wapo wasanii wanaonunua kazi zangu kwa wingi lakini wengine wanaahidi tu hawanunui, nawaomba wanunue ili tusaidiane kuzitangaza na pia tutangaze taifa letu kwa ujumla kutokana na nafasi na majina yetu yalivyo makubwa ndani na nje ya nchi,’’ alisema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles