24.5 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

IGP ataka barua kumkamata Gwajima

Na Brighiter Masaki

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania, IGP Simon Sirro amesema Jeshi la Polisi linaendeshwa kwa maandishi hivyo wanasubiri barua kutoka kwa Waziri wa Afya, Dk. Dorothy Gwajima kuhusu maagizo ya kumkamata Askofu Josephat Gwajima.

Kauli hiyo ya IGP Sirro, amekuja baada ya waziri huyo kuliagiza Jeshi la Polisi na Takukuru kumkamata na kumhoji Mbunge wa Kawe, Askofu Gwajima.

IGP Sirro amesema maagizo hayo yameonekana mtandaoni hivyo wanasubiri agizo rasmi na kutekeleza agizo hilo na wataangalia kama kuna jinai kabla ya kufungua mashtaka mahakamani.

“Hatujapa taarifa rasmi ya maandishi ya kutakiwa kumkamata Gwajima, lakini hata tukiipokea tutachunguza iwapo matamshi yake yanaangukia kwenye jinai, lakini tunaweza kuwashauri wakatatua jambo hili kwa njia za mazungumzo badala ya Polisi.

“Sisi kama polisi hatuna nafasi ya kufanya lolote kumhoji mtu pale anaposema maneno yasiyo na jinai ndani yake,” amesema majibu ya IGP Simon Sirro

Dk. Gwajima ametoa agizo hilo kutokana na kauli za Askofu huyo a kupinga hadharani chanjo ya Uviko-19.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles