22.8 C
Dar es Salaam
Thursday, April 18, 2024

Contact us: [email protected]

Zuma akwama kutoka gerezani

RAIS wa zamani wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, amekwaa kizingiti baada ya rufaa yake ya kutaka aondolewe hukumu ya kifungo cha miezi 15 gerezani kwa kosa la kuidharau mahakama.

Mahakama Kuu nchini humo ndiyo iliyothibitisha kuwa rufaa ya Zuma imetupiliwa mbali, hivyo ataendelea kutumikia kifungo hicho alichohukumiwa Juni, mwaka huu.

Julai, mwaka huu, Zuma mwenye umri wa miaka 79 aliomba adhabu yake ya miezi 15 iangaliwe upya kwa kile alichodai umri wake mkubwa unamuweka kwenye hatari ya kupata Corona akiwa gerezani.

Mwanasiasa huyo aliiongoza Afrika Kusini kuanzia mwaka 2009 hadi 2018 lakini utawala wake huo ulikabiliwa na shutuma nyingi za vitendo vya rushwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles