26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Zitto arudishwa Mahabusu Mburahati

Patricia Kimelemeta, Dar es Salaam

Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe leo Novemba 1, 2018 ameondolewa kituo cha Oysterbay alikokuwa amehifadhiwa na kupelekwa Mahabusu ya kituo cha polisi Mburahati kilichopo Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam.

Uamuzi huo umekuja baada ya jeshi la polisi kufanya upekuzi nyumbani kwake kuanzia saa 2:20 asubuhi hadi saa 5:45 na kumrudisha tena kituo cha Oysterbay.

Wakili wa Zitto, Jebra Kambole amesema kwamba wapo kwenye mchakato wa kuwasilisha maombi ya dhamana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ili mteja wao apate dhamana.

“Tupo kwenye hatua za mwisho za kuwasilisha maombi ya dhamana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ili mgeja wetu aweze kupewa dhamana,” ameeleza Kambole.

 

 

 

 

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles