24.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Z’BAR YATOA ONYO WAUZA MADUKA YA DAWA

Na Suleiman Rashid Omar-Pemba


WIZARA ya Afya na Ustawi wa Jamii ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, imesema haitowavumilia watu wanaowatumia wanafunzi wa shule za sekondari kwa kuuza dawa za binadamu hali ya kuwa hawana taaluma hiyo.

Onyo hilo limetolewa na Ofisa Mdhamini wa Wizara ya Afya Kisiwani Pemba,  Bakari Ali Bakari, alipokuwa shehena za dawa mbalimbali zilizotolewa na UMATI kisiwani hapa ikiwa ni utekelezaji wa mradi wa uimarishaji  afya kupitia huduma Lishe, Uzazi na Usafi wa  Mazingira.

 “Ni jambo lisilokubalika kwa baadhi ya wamiliki wa maduka ya madawa kuwaweka watoto wao washule  kuuzia watu madawa sisi kama wizara ya afya tutahakikisha wale wote wenye mtindo huo tunawakamata,” Bakari

Kutokana na hali hiyo aliiagiza Bodi ya Madawa kufanya ukaguzi kila wakati ili kuhakikisha kila kituo cha afya vikiwemo vinavyomilikiwa na watu binafsi vinafuata masharti yaliyowekwa kwa mujibu wa sheria.

Kwa upande wake Mratibu wa UMATI kisiwani Pemba, Rashid Abdalla Rashid,  alisema lengo la kukabisdhi dawa hizo ni kusaidia vituo vya afya vilivyo ndani ya mradi huo.

Alisema mradi huo una lengo la kuboresha afya ya uzazi na kupunguza ongezeko la maradhi ya kuambukiza pamoja na Vifo vya watoto  katika mkoa wa kaskazini Pemba

Akivitaja vituo vitakavyopatiwa madawa hayo kuwa ni Maziwang’ombe,  Shumba, Vyamboni, Konde na Hospitali za Micheweni, Kojani, Tungamaa, Jadida na Hospitali Wete.

Alisema wakati wa kutekeleza mradi huo inatarajia kujenga vyoo katika Shule ya Kojani na kuweka tangi la maji ilikuondoa tatizo la maji katika shule hio.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles