24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

YOUNG DEE KUPAMBA AFTER SCHOOL BASH LEO

11205845_1702680259954682_1343396100_nTAMASHA la burudani linalohusisha wanafunzi kutoka shule na vyuo mbalimbali linaloitwa After School Bash linafanyika leo kwenye ufukwe wa Escape One jijini Dar es Salaam ambapo nyota mbalimbali wa muziki wakiongozwa na David Genzi ‘Young Dee’ watatumbuiza.

Akipiga stori na Swaggaz kuhusiana na tamasha hilo, Young Dee alisema amejiandaa vya kutosha kuhakikisha
mashabiki wake watakaokwenda kwenye ufukwe huo watapata burudani ya nguvu kutoka kwake.

“Binafsi nimejiandaa poa kuhakikisha kwamba natoa burudani ya kutosha kwa mashabiki wangu, kikubwa watu wote wajitokeze kwa wingi.

Hili ni tamasha la mwisho kwa mwaka huu hivyo lazima tule bata vya kutosha,” alisema Young Dee.

Mbali na Young Dee jukwaa la After School Bash mwaka huu litashambuliwa na nyota wengine kama Jux, Vanessa Mdee, Ruby, Weusi, Stamina, Young Killer, Chemical na Izzo Biznes na wen­gine wengi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles