26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Yanga yazindua Wiki ya Wananchi kwa kishindo

NA MWAMVITA MTANDA

YANGA imezindua kwa kishindo tamasha lake lililopewa jina la Wiki ya Wananchi, ambapo wapenzi, wanachama na mashabiki wa klabu hiyo nchi nzima watafanya shughuli za kijamii.

Tamasha hilo lililozinduliwa jana Dar es Salaam, litafikia tamati Agosti 4, Uwanja wa Taifa jijini humo, ambapo kikosi cha timu hiyo kitakachoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao na mashindano mengine, ikiwemo Ligi ya Mabingwa Afrika kitatambulishwa.

Mbali ya kutambulisha wachezaji, timu hiyo itashuka dimbani kuumana na Kariobangi Sharks ya Ligi Kuu ya Kenya, katika mchezo  wa kirafiki  utakaopigwa kwenye uwanja huo.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Wiki ya Wananchi, Rogers Gumbo alisema, lengo la kunzisha tukio hilo kuwakutananisha wanachama wa Yanga na kufanya shughuli mbalimbali za kijamii, ikiwemo kufanya usafi na kutembelea wagojwa katika hospitali.

“Hii wiki ni muhimu sana kwetu tena ya kihistoria tangu kuanzishwa kwa klabu hii, hivyo naweza kusema itasaidia kuwajenga Wanayanga na kutambua majukumu yao katika jamii,”alisema Gumbo.

Rogers alisema  baadhi ya wanachama wa klabu hiyo leo watasafiri kwenda Zanzibar ambako watakutana na wadau na mashabiki wa huko na kufanya mkutano mkubwa wa wanachama.

Alisema wakiwa huko, watawatembelea wagonjwa na kufanya usafi katika maeneo mbalimbali.

Alisema Wiki ya Wananchi itaenda sambamba na burudani za ngoma za asili.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles