33.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Xi na Kim wakubaliana kuimarisha urafiki wa China, Korea Kaskazini

PYONGYANG, KOREA KASKAZINI

KIONGOZI wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un na mwenzake wa China, Xi Jinping, wamekubaliana kuimarisha urafiki wa mataifa hayo mawili bila kujali mwenendo wa siasa za kimataifa.

Shirika la Habari la Korea Kaskazini limeripoti kwamba viongozi hao wawili wamezungumzia mfululizo wa mipango ya kuimarisha ushirikiano ikiwemo masuala ya kisera wakati wa siku ya mwisho ya ziara ya Xi mjini Pyongyang.

Hata hivyo, hakuna maelezo ya ziada yaliyotolewa kuhusu makubaliano yaliyofikiwa.

Rais Xi ameondoka Korea Kaskazini baada ya ziara ya siku mbili ambayo ni ya kwanza kufanywa na kiongozi wa China katika kipindi cha miaka 14 iliyopita.

Ziara ya Rais wa China nchini Korea Kaskazini imelenga kuonesha mshikamano na taifa hilo linalokabiliwa na shinikizo la vikwazo vya Umoja wa Mataifa kutokana na mpango wake tata wa silaha za nyuklia.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles