30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Wenger kurudi Arsenal, Salah akisepa…

London, Uingereza

Kocha wa zamani wa Arsenal, Arsene Wenger, ni miongoni mwa wadau watakaoungana na kampuni ya Spotify kuinunua klabu hiyo.

Taarifa zimedai Wenger atashirikiana na wachezaji watatu wa zamani wa klabu hiyo ili kumpa nguvu mmiliki wa Spotify, Daniel Ek. CHANZO: BeIN Sports

Lingard kulazimisha kuondoka

KIUNGO wa Manchester United, Jesse Lingard, anatarajia kulazimisha kuondoka zake Old Trafford mwishoni mwa msimu huu.

Lingard anayecheza kwa mkopo West Ham, haoni sababu ya kurudi Man United kwa sababu hana uhakika wa namba chini ya Ole Gunnar Solskjaer. CHANZO: Eurosport

Chelsea wammezea mate Pedraza

KLABU ya Chelsea inavutiwa na mpango wa kumsajili mlinzi wa pembeni wa Villarreal, Alfonso Pedraza.

Endapo watamkosa, Blues watahamishia ‘majeshi’ kwa beki mwingine anayecheza Atalanta ya Italia, Robin Gosens.

CHANZO: Caught Offside

Kigogo afunga mjadala wa Messi

RAIS wa zamani wa Barcelona, Jordi Mestre, amesema hakuna uwezekano wa Lionel Messi kuondoka klabuni hapo.

Messi mwenye umri wa miaka 33, ataongeza mkataba mpya licha ya kutakiwa PSG na Manchester City, kwa mujibu wa Mestre. CHANZO: Talksport

Arsenal chalii kwa Odegaard

REAL Madrid hawamuuzi kiungo wao raia wa Norway anayecheza kwa mkopo Arsenal, Martin Odegaard.

Hilo ni pigo kwa Washika Bunduki kwani wamekuwa wakipanga kumsajili moja kwa moja mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22. CHANZO: AS

Salah akisepa, Sancho anaingia

LIVERPOOL watamgeukia winga wa Borussia Dortmund, Jadon Sancho, endapo watampoteza staa wao, Mohamed Salah.

Salah amekuwa akihusishwa na Barcelona na Real Madrid, hivyo kocha Jurgen Klopp anaona itakuwa ngumu kumbakiza nyota huyo raia wa Misri.

Hata hivyo, changamoto inayoweza kuikumba Liverpool ni dau la Pauni milioni 120 linalotakiwa na mabosi wa Dortmund.

Bellingham mshahara mara mbili Dortmund

ILI kumshawishi asiondoke Borussia Dortmund, klabu hiyo imepanga kuongezea mara mbili ya mshahara wanaompa staa wao, Jude Bellingham.

Hiyo ni katika juhudi zao za kumzuia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 17 asiende Chelsea.

Bellingham amekuwa mchezaji muhimu wa Dortmund tangu alipojiunga na timu hiyo akitokea Birmingham City mwaka jana.

Tottenham kubeba wawili Tottenham

MABOSI wa Tottenham wanajipanga kumsajili beki wa kati wa Fulham, Joachim Andersen, sambamba na kiungo wa Celtic, Ismaila Soro.

Hata hivyo, Tottenham watakabiliana na Manchester United na Chelsea ambazo pia zinamtolea macho Andersen.

Soro, licha ya kwamba amecheza mechi 20 msimu huu, ameingia kikosi cha kwanza cha Celtic mara moja tu tangu Februari, mwaka huu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles