27.1 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Waziri wa Afya atangaza kifo cha kwanza mgonjwa wa corona nchini

Aveline Kitomary, Dar es salaam

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu leo amethibitisha kifo cha kwanza cha mgonjwa wa virusi vya corona ambaye ni mwanamume aliyekuwa akitibiwa katika kituo cha matitabu ya wagonjwa wa corona kilichopo nje ya hospitali ya Mloganzila.

Waziri Ummy amesema mgonjwa aliyepoteza maisha ni Mtanzania mwenye umri wa miaka 49 aliyekuwa akipatiwa matibabu katika kituo hicho.


“Nasikitika kutangaza kifo cha kwanza cha mgonjwa wa Covid -19 hapa nchini kilichotokea alfajiri ya leo tarehe Machi 31, wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika kituo cha Mloganzila Dar es salaam.


“Marehemu ni Mtanzania mwenye umri wa miaka 49 ambaye pia alikuwa akisumbuliwa na maradhi mengine, tunamwomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi na tunatoa pole kwa ndugu hasa wa marehemu,” amesema Waziri Ummy.


Hadi sasa jumla ya wagonjwa waliopata maambukizi ya Covid-19 nchini ni 19, aliyepona ni mmoja na aliyefariki dunia ni mmoja.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles