24.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Waziri Mkuu wa Uingereza amfukuza kazi waziri wake wa ulinzi

Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amemfukuza kazi Waziri wake wa Ulinzi Gavin Williamson.

Waziri huyo wa Ulinzi amefukuzwa kazi kwa sababu ya kutoa siri juu ya mkutano wa baraza la usalama wa taifa ambapo mawaziri waliijadili kampuni ya China ya mawasiliano ya Huawei.

Kufukuzwa kwa Williamson, ambaye amekanusha vikali kuhusika na uvujishaji wa taarifa hizo, ni pigo jingine kwa May, ambaye nafasi iko mashakani baada ya kushindwa kufanikisha mchakato wa Brexit.

Penny Mordaunt ameteuliwa kuwa waziri mpya wa ulinzi na hivyo kuwa mwanamke wa kwanza nchini Uingereza kushika wadhifa huo. Hapo awali alikuwa waziri wa misaada ya maendeleo inayotolewa kwa nchi za nje.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles