24.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Waziri Mkuu kujiuzulu

VALLETA, MALTA

WAZIRI Mkuu wa Malta, Joseph Muscat ameliarifu taifa lake kwamba atajiuzulu mwezi ujao, baada ya shinikizo kutoka kwa wananchi wenye hasira, wanaotaka kujua ukweli kuhusu mauaji ya mwandishi wa habari za uchunguzi,, Daphne Caruana Galizia aliyeuawa na bomu lililotegwa ndani ya gari lake mwaka juzi.

Muscat alisema amemfahamisha rais wa nchi kuwa Januari 12, 2020 atajiuzulu kama kiongozi wa chama tawala cha Labour, na siku zitakazofuata atauachia pia wadhifa wake wa waziri mkuu.

Kabla ya tangazo lake, watu 20,000 waliandamana mbele ya jengo la mahakama mjini Valleta, wakimtaka aondoke madarakani.

Muscat alisema katika hotuba yake kwamba ametimiza ahadi aliyoitoa kwa wananchi miaka miwili iliyopita, kwamba haki itatendeka kuhusu mauaji dhidi ya mwandishi Galizia.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles