26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Watumishi Zimbabwe walazimishwa chanjo

SERIKALI ya Zimbabwe imeweka wazi kuwa mtumishi wa umma ambaye atapuuzia na kutopata chanjo ya Corona hataruhusiwa kuingia ofisini.

Aidha, taarifa ya Serikali haijafafanya kama mtumishi asiyechanjwa atapoteza ajira au ataendelea majukumu yake ya kazi akiwa nyumbani.

Kwa mujibu wa Waziri wa Habari, Monica Mutsvangwa, Serikali imewapa muda watumishi kuhakikisha wanapata chanjo, kabla ya kuanza kusimamia utekelezaji wa agizo hilo.

Katika kile kilichoelezwa na Wizara, asilimia 90 ya wagonjwa walioko hospitali wakisumbuliwa na Covid ni wale waliopuuzia chanjo.

Kufikia sasa, Zimbabwe inatajwa kupokea maambukizi mapya 145 kila siku na jana viliripotiwa vifo saba.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles