27.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Watumishi wa Umma marufuku kudai nyongeza ya mshahara

Arodia Peter, Dodoma

Serikali imesema watumishi wa umma hawapaswi kuomba nyongeza ya mwaka ya mshahara, bali Serikali ndiyo yenye uamuzi wa kutoa au kutotoa nyongeza.

Hayo yamesemwa bungeni leo Mei 14, na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na utawala bora) Dk. Mary Mwanjelwa wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Tunza Issa Malapo (Chadema).

Mbunge huyo alitaka kujua serikali inatumia sheria ipi kutowapa wafanyakazi stahiki zao zinazohusu kupandishwa madaraja, na ongezeko la mwaka.

Katika majibu yake, Dk. Mwanjelwa amesema kwa mujibu wa kanuni E.9 (1) ya kanuni ya kudumu katika utumishi wa umma za mwaka 2009, toleo la tatu, nyongeza ya mwaka ya mishahara haipaswi kuombwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles