24.4 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

WATUMIA BARABARA KUONGEZEWA TOZO

Gabriel Mushi, Dodoma

Serikali imesema ina mpango wa kuongeza tozo kwa watumiaji wa barabara ili kuiongezea fedha Wakala wa Barabara Vijijini (Tarura).

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema hayo bungeni leo wakati akihitimisha mjadala wa wabunge waliochangia katika hotuba ya wizara hiyo.

Amesema Tarura imepewa asilimia 30 ya bajeti na Wakala wa Wakala wa Barabara nchini (Tanroads) asilimia 70 kwa sababu Tanroads inasimamia mtandao mkubwa wa barabara kuliko Tarura.

Aidha, aliwataka wananchi kutumia sekta ya mawasiliano vizuri kwa maendeleo ya kichumi.

“Niwaombe watumia miundombinu ya mawasiliano kutumia kwa maslahi ya taifa na si uchochezi au picha chafu,” amesema Profesa Mbarawa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles