WASHINGTON, MAREKANI
Watoto wawili wa kiume wa Rais Donald Trump wamewashutumu wanachama wa Republican kwa kutomuunga mkono rais anapokabiliwa na ushindani mkali kutetea mhula wa pili madarakani.
Mwana mkubwa wa, Trump Don Jr alikosoa chama kwa kuwa “dhaifu”. Ndugu yake Eric alionya: “Wapiga kura wetu hawatawahi kuwasahau mkijifanya wanyonge!”
Hatua hiyo inaasharia ya mgawanyiko ulioibuka kati ya washirika wa Trump ndani ya chama.
Ushandani mkali umeshuhudiwa lakini mgombea wa Democratic Joe Biden anyone kana kuelekea kupaya ushindi.
Trump ameapa kupinga matokeo ya uchaguzi huo mahakamani akitilia shaka shughuli ya kuhesabu kura inavyoendeshwa akidai kumekuwa na visa vingi vya udanganyifu.
Wanasiasa wa ngazi ya juu katika chama cha Republican kama vile seneta wa Utah Mitt Romney na Gavana wa Maryland Larry Hogan wameonya hatua ya kuhujumu mchakato wa kidemokrasia.