25.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

WATOTO 800 HUUGUA SARATANI KWA MWAKA

NA HARRIETH MANDARI-DAR ES SALAAM

WATOTO 800 ambao  asilimia 30 huugua saratani , kati ya watoto 2,500 wanaofikishwa katika vituo vya afya kupima ugonjwa huo.

Kutokana na hali hiyo, wazazi wameshauriwa kuwafikisha watoto wao katika vituo vya afya kupima ugonjwa huo kwa vile  kundi hilo limeelezwa kusahaulika   na badala yake wengi wao hufikishwa  wakiwa na hali mbaya.

Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa Asasi isiyo ya Serikali ya  Marafiki wa Watoto wenye Saratani  Tanzania, Janeth Manoni, alikuwa akizungumzia uhamasishaji na  utoaji elimu juu ya saratani kwa watoto jana.

Uhamasishaji huo utahusisha kupima afya hasa ya magonjwa yasiyoambukiza kwa watoto na utafanyika  Februari 18 mwaka huu katika viwanja vya Don Bosco,   Dar es Salaam.

Alisema elimu juu ya ugonjwa huo kwa watoto inatakiwa kutolewa nchini kote si tu kwa wazazi lakini pia hata watoa huduma kwa sababu  bado hawana uelewa.

“Utakuta mzazi anapoleta mtoto mwenye saratani anasema amekuwa akimpeleka   hospitali na kueleza dalili ambazo mtoto anapata  na huishia kupata dawa zisizo sahihi na matokeo yake ugonjwa kuenea zaidi,” alisema.

Alisema asasi hiyo kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Dini la Mtakatifu  Don Bosco na wadau mbalimbali  wakiwamo madaktari, imeandaa mkutano huo    ambako pia itakuwapo michezo kwa watoto hao.

Naye Mhamasishaji wa Asasi hiyo,  Renidius Rwezaula alisema  madaktari 30  watakuwapo   kutoa huduma ya upimaji afya kwa watoto na kutoa elimu  bure.

“Wakati umefika kwa Watanzania kuanza kupima afya bila kusahau watoto wetu mara kwa mara  kwa kuwa ugonjwa wa saratani unapoanza hauna maumivu  jambo ambalo husababisha wagonjwa wengi kuletwa hospitali wakiwa wameathirika kwa kiasi kikubwa,” alisema.

Rwezaula alisema mgeni rasmi katika kongamano hilo atakuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi.

Vilevile   watakuwapo   viongozi wa dini ambao pia watasaidia kutoa ushauri  wa roho kwa wagonjwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles