Na AVELINE KITOMARY-DAR ES SALAAM
MGANGA Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dk. Yudas Ndugile, amesema katika mkesha wa Krismasi watoto 212 wamezaliwa katika mkoa huo.
Gazeti la MTANZANIA pia lilipita katika hospitali mbalimbali mkoani ili kupata taarifa za uzazi zaidi ambapo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili watoto waliozaliwa katika mkesha wa Krismasi walikuwa sita, wanne kutoka Upanga na wawili Mloganzia .
Ofisa habari wa Muhimbili, John Stephen, alisema watoto waliozaliwa wote ni wakike na wamezaliwa kwa njia ya kawaida huku afya za watoto na wazazi zikiendelea vizuri.
Naye Ofisa Muuguzi wa Hospitali ya Temeke, Hamisa Sadick alisema katika hospitali hiyo watoto waliozaliwa ni 14, watoto pamoja na wazazi hali zao zinaendelea vizuri.
“Kati ya hao watoto tisa walizaliwa kawaida wa kiume ni wanne na wakike ni watano na waliozaliwa kwa upasuaji wako watano ambapo wawili ni wakike na watatu niwakiume wote zalizao ni njema,”alisema Hamisa.
Kwa upnade wa Hospitali ya Mwananyamala katika mkesha wa krismasi jumla ya watoto 19 walizaliwa kati ya hao 14 ni wakike na watano ni wakiume.
“Watoto waliozaliwa kwa njia ya kawaida wakike ni 12 na wakiume ni wane na waliozaliwa kwa upasuaji wawili walikuwa wakike na mmoja wakiume lakini wote hali zao zinaendelea vizuri,” alisema Muuguzi Abdul Mohamed.