27.9 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Watatu wauawa wakijaribu kuwatoroka polisi

Na Gurian Adolf-Sumbawanga

POLISI wilayani Nkasi, mkoani Rukwa, imewaua kwa kuwapiga risasi watu watatu wakati wakijaribu kutoroka wakiwa chini ya ulinzi.

Tukio hilo lilitokea Septemba 20, mwaka huu saa 5 usiku katika Barabara ya Nkundi kuelekea Kijiji cha Kate, wilayani humo, baada ya watu hao waliokuwa wakituhumiwa kufanya mauaji ya watu sita kwa kuwakata mapanga na mashoka baada ya kuruka katika gari la polisi na kutaka kukimbia.

Akitoa taarifa ya tukio hilo mwishoni mwa wiki, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando, aliwataja waliouawa kwa kupigwa risasi na polisi kuwa ni Nching’wa Njige (44), Dashina Ngeseyamawe (46) ambao ni wakazi wa Kijiji cha Ntalamila pamoja na Joseph Jiuke(34) mkazi wa Kijiji cha Chonga.

Alisema watu hao walikuwa wamepakiwa kwenye gari la polisi ili waende kuonesha watuhumiwa wenzao ambao walikuwa wakitafutwa kwa kushiriki kufanya mauaji ya watu sita kwa kuwakata mapanga na shoka kutokana na imani za kishirikina.

Kamanda Kyando alisema waliokuwa wanatafutwa ni Mabula Sokoni, Said Tongela pamoja na mganga wa jadi, John Luchwela ambaye aliwapa dawa ili wasikamatwe baada ya kufanya mauaji hayo.

Wakiwa wanaelekea wanakopatikana watuhumiwa hao wengine, ndipo waliporuka katika gari la polisi ili watoroke kitendo kilichosababisha polisi kuwafyatulia risasi.

Kabla ya kuuawa kwa watuhumiwa hao waliokamatwa kufuatia msako ulioanza Julai 1 na walipohojiwa na polisi walikiri kufanya mauaji ya watu sita kwa kuwakata mapanga na mashoka.

Waliwataja  waliowaua kuwa ni Naomi Ng’wanamayunga, mkazi wa Kijiji cha Ntuchi,  Samweli Seki, mkazi wa Kijiji cha Ntalamila, Jibuta Majebele, mkazi wa Kijiji cha Mkole, Odoviko Sumuni, Salome Kisinza, wakazi wa Kijiji chalachima na Said Matenga mkazi wa Kijiji cha Mwai kwa madai kuwa ni wachawi.

Awali kabla ya kuuawa kwa kupigwa risasi na polisi, watu hao katika mahojiano walikiri pia kuwaua watu zaidi ya 15 kwa nyakati tofauti katika mikoa ya Rukwa, Katavi na Simiyu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles