31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Wasichana waogeshwa dawa kuvutia wanaume

BENJAMIN MASESE-MWANZA

SERIKALI imeombwa kupiga marufuku vitendo vya baadhi ya wazazi kuwapeleka  mabinti wao wenye umri kati ya miaka  10 hadi 15  kuogeshwa dawa la kuvutia wanaume maarufu ‘samba’ kwa kuwa  vinachochea maambukizi ya virusi vya Ukimwi na mimba za utotoni.

Ombi hilo, limetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Kivulini linalojihusisha  kupinga ukatili kwa watoto na wanawake, Yassin Ally.

Alisema  vitendo hivyo vinakwenda kinyume na mikakati ya Serikali ya kutokomeza Ukimwi na mimba za utotoni.

Alisema  vitendo hivyo, vinafanyika kwa wingi Mkoa wa Shinyanga  na kufafanua hivi karibuni alikwenda kutoa semina kwa baadhi ya shule ndani na kuelezwa wanafunzi wa kike wamekuwa wakikosa masomo kutokana na kwenda kuogeshwa.

“Wikiiliyopita nilikwenda Mkoa wa Shinyanga, nilifika baadhi ya shule na kukuta wasichana wenye umri kati ya miaka 10 hadi 15  ni watoro, nilipodadisi sababu ya kushindwa kufika niliambiwa wanakwenda kuogeshwa dawa za mvuto maarufu Samba.

“Cha ajabu walimu wanajua kabisa, watendaji wa vijiji, vitongoji na hata waratibu elimu wanafahamu lakini wanashindwa kuchukua hatua ili kukomesha  mila na desturi za ajabu ambazo zinasababisha watoto kuingia kwenye  maradhi na  mimba za utotoni.

“Wito wnagu Serikali kupitia kwa wakuu wa mikoa, makamanda wa polisi, wakuu wa wilaya na wakurugenzi wapige marufuku vitendo hivyo na wafuatilie kwa ukaribu na kuwachukulia hatua wazazi ambao watabainika kujihusisha na imani potofu, haiwezekani ukamvutia mwanaume kwa dawa ili apende binti, acheni  binti akifikisha umri atachagua mwanaume  anayempenda,”alisema.

Alisema vitendo hivyo, vinaibuka mikoa ya kanda ya ziwa kutokana na kushamiri kwa waganga wa jadi ambao wamejiegesha  katika taaluma hiyo, lengo kubwa ni kutafuta kipato.

Alisema vitendo hivyo kama vitaendelea kuachwa bila kuwekewa adhabu kali,  itakuwa kazi ngumu kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake ambao mwishowe huishia kwenye maradhi yakiwamo Ukimwi, mimba za utotoni na utelekezaji familia.

Hivi karibuni Shirika  la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Masuala ya Wanawake (UN  Women),  liliwakutanisha wazee 225 maarufu wa mila kutoka mikoa  tisa ikiwa ni sehemu ya kuisaidia Serikali ya Tanzania  kutimiza malengo ya mikataba ya kimataifa na kikanda  ya kukomesha vitendo ukatili wa jinsia na kuleta usawa ndani ya jamii.

Akizungumza katika ufunguzi wa semina kwa wazee hao waliokutanishwa jijini Mwanza, Ofisa Elimu na Uhamasishaji kutoka UN Women, Lucy Tesha alisema  wadau wakubwa wa mashirika ya kimataifa ni Serikali kwa pamoja hushirikiana masuala ambayo yamewekwa katika mikakati ya kimaendeleo kwa  kuwafikia walengwa ambao ni  wananchi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles