30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Warrinka ajitoa kushiriki Olimpiki

Stan WawrinkaZURICH, USWISI

NYOTA wa mchezo wa tenisi nchini Uswisi, Stan Wawrinka, amejiondoa kushiriki michuano ya Olimpiki ambayo inatarajia kuanza kutimua vumbi kesho nchini Brazil.

Mchezaji huyo ambaye anashika nafasi ya nne kwa ubora wa tenisi kwa upande wa wanaume duniani, amejiondoa kushiriki mashindano hayo makubwa duniani baada ya kupata majeraha katika michuano ya Rogers Cup iliyofanyika huko Toronto nchini Canada.

Nyota huyu aliondolewa katika hatua ya nusu fainali baada ya kufungwa na Kei Nishikori mwezi uliopita na kutokana na ushauri wa daktari wake ameamua kujiondoa katika michuano hiyo baada ya kuhisi maumivu.

“Nilikuwa na lengo la kuandika historia mpya katika michuano ya Olimpiki, lakini lengo langu haliwezi kukamilika kutokana na kusumbuliwa na maumivu, hivyo nimeona bora nijitoe katika michuano hiyo,” alisema Warrinka.

Wachezaji wengi mashuhuri wa mchezo huu wa tenisi wamejiondoa kushikiri michuano hiyo ikiwemo Roger Federer, Marcos Baghdatis, kutokana na kusumbuliwa na majeraha.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles