31.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, March 18, 2025

Contact us: info@mtanzania.co.tz

Waogeleaji 14 kuiwakilisha Tanzania nchini Misri

Na Mwandishi Wetu

JUMLA ya waogeleaji 14 wameunda timu ya Taifa kujiandaa na mashindano ya vijana ya kuogelea ya Afrika yatakayofanyika kuanzia April 30, hadi Mei 3, mwaka huu nchini Misri.

Kwa mujibu wa taarifa  iliyotolewa leo na Msemaji wa Chama cha Kuogelea Tanzania (TSA), Sebastian Kolowa timu hiyo imeshaanza maandalizi ya michuano hiyo kuhakikisha inakwenda kushiriki na kufanya vizuri.

“Kati ya waogeleaji hao, saba ni wanaume na wengine saba ni wanawake. Uchaguzi wa kikosi umetokana na mashindano mbalimbali yaliyopita ikiwemo iliyofanyika wiki mbili zilizopita,”amesema.

Waogeleaji hao ni Romeo Mwaipasi, Aryan Bhatt, Mark Tibazarwa, Austin Okore, Christian Fernandes, Enrico Baretto, Sahal Haarunani.

Wengine ni Filbertha Demello, Lina Goyayi, Bridget Heep, Natalia Ladha, Amylia Chali, Aliyana Kachra na Aminaz Kachra. 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
595,000SubscribersSubscribe

Latest Articles