24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Wanyama amkaribisha Samata EPL

NA SOSTHENES NYONI-DAR ES SALAAM

KIUNGO wa kimataifa wa Kenya , Victor Wanyama amemkaribisha  mshambuliaji Mbwana Samatta kukipiga  LigI Kuu ya England msimu ujao.

Samatta ambaye ni mshambuliaji wa timu ya KRC Genk inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza nchini Uholanzi, ameingia kwenye rada ya timu saba zinazoshiriki Ligi Kuu ya England zikiwania saini yake ili azitumikie msimu ujao.

Timu hizo ni pamoja na Leicester City, Cardiff, Westham United, Brighton, Aston Villa, Watford na Burnley ambazo kama ofa zao zitakubaliwa na  Genk, moja wapo itamsajili Samatta.

Mbali ya timu hizo za England, Lazio ya Italia na Lyon ya Ufaransa pia zipo katika mbio za kumwania mshambuliaji huyo wa zamani wa TP Mazembe ya DRC na Simba ya hapa nchini.

Samatta na Wanyama walikutana katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika(Afcon)inayoendelea kushika kasi nchini Misri huku kila mmoja akilipigania taifa lake.

Kwa upand wa Samatta alikuwa nahodha wa kikosi  cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ iliyoshiriki fainali za Afcon kabla ya kutupwa nje hatua ya makundi.

Kama ilivyo kwa Samatta, ambaye  anakipiga Tottenham inayoshiriki Ligi Kuu ya England,  alikuwa nahodha wa kikosi cha Kenya(Harambee Stars), kilichoshiriki  fainali za mataifa ya Afrika(Afcon)zinazoendelea nchini Misri kabla ya kuondolewa hatua ya makundi.

Mara baada ya Taifa Stars kuondolewa katika michuano ya Afcon, Samatta aliandika maneno haya kupitia akaunti yake ya  instagram; “Ilikuwa ni nafasi nzuri kucheza na mmoja wa wachezaji Bora na wa mfano wa kuigwa katika ukanda huu wa Africa mashariki, tunajivunia uwepo wako ndani ya East Africa.”

Maneno ya Samatta yalionekana kumgusa Wanyama ambaye naye  kupitia akaunti yake ya instagram jana aliandika;”Nashukuru Sana Kaka yangu,na ni matarajio yangu kukuona premierleague (Ligi Kuu England) msimu ujao tuendelee kupeperusha bendera ya East Africa(Afrika Mashariki).

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles