24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Wanaume waanza kuandika wosia

FRANCIS GODWIN, IRINGA

WAKAZI wa Kata ya Mlowa wilayani Iringa,  wameanza  kuandika wosia    mapema kama kinga ya kuwalinda  dhidi ya vitendo  vya manyanyaso wajane  na  watoto wanaowaacha, baada ya  kufariki  dunia.

Wakizungumza  juzi  kwa nyakati  tofauti, wakati  mahojiano maalumu na    timu ya   tathimini,   baada ya mafunzo yaliyotolewa na Shirika  na shirika  lisilo la  kiserikali la Iringa Civil Society Organizations (ICISO –UMBRELLA),  chini ya  ufadhili wa miradi ya  Internews ,USAID na fhi360,wakati hao, walisema   kabla ya  elimu  kutolewa  hakuna  mwanaume  aliyekuwa  tayari  kuandika wosia.

Mkazi wa Kijiji cha Nyamahana, Daud Ndihungule alisema   pamoja na kutokuwa na utalaamu wa kuandika wosia, ameanza kuorodhesha mali zake na kuweka mgawanyo kwa familia yake.

“Nilianza  na  kuandaa na kumbukumbu ya maisha yangu, niliyozaliwa na kuweka kumbukumbu  sahihi ya mke  wangu halali  ninayeishi nae, idadi ya watoto  na mwisho  kuandika mali ambazo tunazimiliki.

Mimi,mke  wangu na  watoto tumeshiriki kuchuma mahali, nimeona ni vizuri nikaweka utaratibu mzuri nikiwa bado niko hai,”alisema Ndihungule

Alisema kabla ya kupata  elimu   ya haki  sawa  katika  umiliki wa ardhi,mirathi na  wosia,  wanaume  wa  kijiji  hicho  wameonyesha  kubadilika  kwa  kuishi  tofauti na wake  zao.

Alisema bila kuandika mirathi husababisha migogoro mingi kutokana na mali zinazoachwa.

“Pamoja na  kuwa mjane  na  watoto  ndiyo,  wanaopaswa kuangaliwa zaidi katika mgawanyo wa mali, mashemeji  walikuwa  wakichangamkia  kuchukua mali  za marehemu,”alisema.

Mkazi wa Mafuluto, John  Kidanyali alisema  bado  kuna haja ya  asasi ya  ICISO  kuendelea kutoa elimu mara kwa mara   jinsi ya  kuwahamasisha  wanaume na hata  wanawake  kuandika wosia.

“ Ujue kijijini  tunaishi kama  ndugu  wa familia mmoja, ukitokea msiba  kijiji  kizima tunafika kushiriki,wakati wa  kumaliza  misiba  tunashuhudia  mambo mengi,”alisema.

Kwa upande wake, mkazi wa Nyamahana, Christina  Nzala aliomba elimu  kuendelea  kutolewa kwa maeneo mengine maana juu ya umiliki  wa mali kwa  wanawake na watoto.

Kaimu  Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Mafuluto, Ditrick Kaywanga  alisema  kutolewa  elimu  hiyo kumepunguza migogoro.

Katibu Mtendaji wa ICISO, Raphael Mtitu  alisema shirika lake  limekuwa  likifanya kazi mkoa mzima wa Iringa.

Alisema lengo la kufanya  tathimini ya mafunzo  hayo, ni kutaka  kujua kama elimu  hiyo  iliwafikia ama haikuwasaidia lakini walichojifunza ni  kuwa elimu  hiyo  imeweza  kuibua hamasa  kubwa ya  wanawake waliodhurumiwa mahali zao.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles