26.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Wanasayansi wadai povu la chura ni tiba

Povu la churaGLASGOW, UINGEREZA

WANASAYANSI nchini Uingereza wamesema povu linalotolewa na vyura wadogo kwa ajili ya kulinda mayai yao linaweza kuponya majeraha ya wagonjwa walioungua kwa moto.

Pia wanaamini kuwa povu hilo linaweza kukusanywa na kusaidia mchakato wa matibabu kama kizuizi baina ya bandeji na ngozi iliyoungua.

Watafiti kutika Chuo Kikuu cha Strathclyde wameanza utafiti juu ya povu hilo linalotolewa na vyura wadogo kutoka kwenye kisiwa cha Tungara, huko Trinidad.

Vyura hao hutoa povu la urefu wa sentimita 5 kulinda mayai yao dhidi ya magonjwa na hali ya hewa kwa wastani wa siku tano.

Povu hilo limetengenezwa kwa aina tano za protini.

Doctor Paul Hoskisson na wenzake wanasema wameweza kuzichunguza aina nne za protini zinazopatikana kwenye povu hilo na kuchanganya na dawa zao ili kuipata tiba husika.

Watafiti hao watawasilisha kazi yao katika mkutano wa mwaka wa kituo cha uratibu wa shughuli za utafiti wa viumbe hai -Microbiology Society- utakaofanyika Liverpool.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles