27.9 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

WANANCHI WAWALALAMIKIA WAHUDUMU KITUO CHA AFYA

 

Na DERICK MILTON


WANANCHI wa Kijiji na Kata ya Ngulyati Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi   wamedai kuwapo  mchezo mchafu kutoka kwa wahudumu wa Kituo cha Afya Ngulyati kuandika taarifa za wagonjwa hewa.

Madai ya hayo ya wananchi yalitolewa juzi mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,  Antony Mtaka kwenye mkutano wa hadhara ulifanyika mjini Ngulyati.

Wananchi hao   walisema wahudumu hao wamekuwa wakifanya hivyo ili kutumia dawa kwa matumizi yao binafsi  huku wazee wakinyimwa huduma za matibabu bure kama inayotakiwa.

Mmoja wa wananchi hao, Ramadhani Kuyege, alisema imekuwapo tabia ya wahudumu wa afya katika kituo hicho kuandika taarifa za wagonjwa hewa.

Alisema watumishi hao pia   wamekuwa wakitumia dawa hizo kinyume na malengo yaliyokusudiwa, hali ambayo  imesababisha  kituo hicho kukosa  dawa kwa muda mrefu.

“Huu mchezo ni mkubwa  kwenye hiki kituo, wanaiba dawa wanapeleka kwenye maduka yao na nyingine wanawauzia wenye maduka ya dawa na sisi wananchi tunakosa tunabaki kuhangaika kila siku,” alisema Kuyege.

Minza Maduhu alidai kuwa kila mara kituo hicho cha afya kimekuwa kikosa dawa na wamekuwa wakiambulia dawa moja tu  ya Panadol.

“Sisi wazee kila siku tunafukuzwa, tunaambiwa lazima tutoe fedha hakuna huduma za bure wakati kila siku viongozi wanatueleza wazee wanapata huduma bure.

“Kituo hiki hakina dawa kila siku wagonjwa wananunua dawa kwenye maduka ya dawa muhimu,” alisema Minza.

Kutokana na malalamiko hayo, RC alimwagiza Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga, kumwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji kumpelekea  taarifa ya matumizi ya Sh milioni 10 ambazo zinatolewa na Wizara ya Afya kwenye kituo hicho.

“Kituo hiki kipata pesa kila mwaka Sh milioni 10 kwa ajili ya kuboresha huduma za afya… niagize kufikia Jumatatu mkurugenzi afike ofisini kwangu kuniletea taarifa ya matumizi ya fedha hizo,” alisema Mtaka.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles