23.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

Wanafunzi 100 wasomea darasa moja

ndalichako
Dk. Joyce Ndalichako

 

NA RAYMOND MINJA, IRINGA

ZAIDI ya wanafunzi 100 wa Shule ya Msingi Image wilayani Kilolo,  wanalazimika kukaa darasa moja kutokana na upungufu wa madarasa uliochangiwa na uchakavu wa majengo ya shule hiyo.

Shule hiyo yenye wanafunzi 761 inahitaji vyumba 18 vya madarasa lakini hadi sasa ina vyumba tisa na vyumba vitatu tu ndivyo vinatumika.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Osideus Lukas, alisema  hayo jana baada ya kupokea msaada wa mabati 50 kwa ajili ya kuezeka madarasa mawili.

Mabati hayo  yalitolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM)  wa Mkoa huo, Jesca Msambatavangu.

Lukas alisema   hali ya shule hiyo kwa sasa si ya kuridhisha kutokana na uchakavu wa majengo.

Alisema  hivi karibuni Idara ya Ukaguzi ya Kanda ilivifunga vyoo vya wanafunzi wa kiume vya shule hiyo kwa kuwa vimejaa na wanafunzi hao kulazimika kutumia vyoo vya wanafunzi wa kike.

“Shule yetu ina mazingira magum,u kwa kweli tunahitaji watu wengine kama alivyoguswa huyu mama.

“Mbali na madarasa   pia tuna uhaba wa vyoo kwa sababu  hivi karibuni wakaguzi walikuja na kutuamuru kufunga vyoo vya wavulana kwa kuwa vilikuwa vimejaa hivyo kwa sasa wavulana wanatumia choo kimoja na wasichana,” alisema.

Mwenyekiti wa Kamati ya shule hiyo, Petro Mkenja alisema mabati hayo yatasaidia kuezeka jengo la vyumba viwili vya madarasa lililokuwa wazi.

Aliwataka watu wengine kuiga mfano wake katika kusaidia jamii.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles