26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Waliokufa katika mashambulio Sri Lanka wafikia 290

COLOMBO, Sri Lanka

SERIKALI imesema  idadi ya vifo vya watu katika mashambulio ya kujitoa muhanga  yalitokea juzi  kanisani na hoteli za  fahali imeongezeka na kufikia 290.

Mbali na taarifa hiyo maofisa hao wa serikali walisema   mashambulio hayo yaliratibiwa na mitandao ya ugaidi ya kimataifa.

Walilishutumu kundi dogo la wapiganaji wa Jihadi linaloitwa  National Towheed Jamath kuhusika na mashambulio hayo yaliyosababisha pia watu 500 kujeruhiwa.

Mpaka mapema jana  hakuna hata kikundi kimoja  kilichojitokeza kudai kuhusika nayo na polisi wanawashikilia watu 24 .

“Hatuwezi kuamini mashambulio haya yamefanywa na kundi la watu waliopo nchini humu,” alisema msemaji wa Baraza la Mawaziri, Rajitha Senaratne.

“Kusingekuwapo na matandao wa kimataifa mashambulio haya yasingefanikiwa,”aliongeza msemaji huyo.

Kwa upande wake Rais wa nchi hii,  Maithripala Sirisena, ameziomba jumuiya za kimataifa kusaidia kuwasaka waliopanga na kufanya mashambulio  hayo.

“Taarifa za  intelijensia zinaonyesha   kuna mtandao wa ugaidi kutoka nje ya nchi ambao umeshirikiana na wa hapa. Hivyo rais anaomba ushirikiano na mataifa ya nje,”ilieleza taarifa ya ofisa ya rais.

Mapema juzi, Waziri Mkuu,  Ranil Wickremesinghe, alieleza kuwa awali kulikuwapo na taarifa   kwamba mashambulio hayo yangefanyika, lakini taarifa hizo hazikuchukuliwa kwa uzito.

 Katika hatua nyingine, Rais Maithripala Sirisena ametangaza hali ya dharura kuanzia jana  usiku hadi leo.

Taarifa ya Kitengo cha Habari cha Serikali   ilieleza kuwa Serikali imeamua kutangaza sheria inayolenga kuzuia ugaidi ambayo itaanza kuheshimiwa kuanzia jana usiku.

Taarifa hiyo ilifafanua kuwa hatua hiyo itahusiana tu na shughuli za kuzuia ugaidi, na haitaingilia uhuru wa watu wa kutoa mawazo yao.

Msemaji wa serikali mjini  hapa,  Rajitha Senaratne alisema  serikali ya Sri Lanka inaamini   kundi lenye itikadi kali la   lijulikanalo kama Nationa Thowheeth Jama’ath (NTJ) ndilo limefanya shambulio hilo  na ameongeza kuwa uchunguzi ulikuwa ukifanyika kuangalia iwapo kundi hilo lilipata msaada kutoka nje ya nchi.

Nyaraka zilizoonwa na Shirika la Habari la Ufaransa (AFP) zinaonyesha kuwa polisi ilitoa onyo Aprili 11 mwaka huu  kwamba shirika la kijasusi la nchi ya kigeni lilikuwa limeripoti kwamba NTJ ilikuwa ikiandaa njama ya kushambulia makanisha na ubalozi wa India.

Hata hivyo hakuna mengi yanayojulikana kuhusu kundi la NTJ, ambalo siku zilizopita lilihusishwa na kufanya uharibifu kwenye sanamu za madhehebu ya Buddha.

 Chanzo cha habari kutoka jeshi la polisi kimeeleza kuwa watu 24 waliokwisha kukamatwa wakishukiwa kuhusika na mashambulio ya siku ya Pasaka wana uhusiano  na kundi hilo lakini hakufafanua zaidi.

Kutokana na shambulio hilo la umwagaji mkubwa wa damu, Sri Lanka iliifunga mitandao mingi ya  jamii, ikiwamo Whatsapp na Facebook, hatua inayodhihirisha kupungua kwa imani katika makampuni hayo mawili makubwa ya Marekani, kuweza kuchuja taarifa za uchochezi.

Mitandao hiyo miwili pamoja na Instagram imeshutumiwa kusambaza habari za uongo. Mtandao wa twitter haukuathiriwa na hatua hiyo.

Ghasia za  dini

Serikali ilihofu kuwa kuenea kwa ujumbe wenye hasira kungechochea ghasia zaidi katika  kisiwa hiki ambacho wakazi wengi wa Wabuddha, lakini pia yakiwapo makundi ya makubwa ya Waislamu, Wakristo na Wahindu.

Hii si mara ya kwanza kwa Sri Lanka kuifunga mitandao ya  jamii. Machi 2018 serikali ya nchi hiyo iliizuia kwa wiki nzima mitandao ya Whatsapp, Facebook na mitandao mingine, kwa hofu kwamba ilikuwa ikiendeleza kampeni ya chuki dhidi ya Waislamu katika jimbo la katikati mwa nchi hiyo

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles