25.8 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

Wakurugenzi hawana mamlaka na fedha za mfuko wa jimbo

Arodia Peter, Dodoma

Wakurugenzi wa halmashauri nchini hawaruhusiwi kutumia fedha za mfuko wa jimbo bila idhini ya mwenyekiti wa mfuko huo ambaye ni mbunge.

Kauli hiyo imetolewa bungeni leo Jumatatu Mei 13, na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mwita Waitara wakati akijibu swali la Mbunge wa Konde, Khatibu Said Haji (CUF).

Katika swali lake, mbunge huyo alitaka kujua kuhusu umuhimu wa Serikali kuongeza viwango vya fedha ili kuleta ufanisi.

Aidha, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Wenye ulemavu, Jenista Mhagama, amesema serikali itatoa waraka mpya kuhusiana na fedha hizo kuwakumbusha wakurugenzi kwamba hawana mamlaka na fedha hizo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles