30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Wajumbe waambukizwa Corona India

New Delhi, India

Waziri wa mambo nje Nchini India Subramanyan Jaishankar amethibisha kuwa wajumbe wanaohudhuria mkutano wa G7 jijini London wakutwa na maambukizi ya Virusi vya corona.

Waziri Jaishankar ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii “Twitter” na kuongezea kuwa wajumbe hao kwa sasa wamejitenga na watahudhuria mkutano huo kupitia mtandao.

Afisa wa serikali ya Uingereza alisema washiriki wawili walipimwa na kupatikana na Corona baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kila siku katika mkutano huo.

Mkutano huo wa mataifa ya G-7 unaingia siku yake ya mwisho huku mawaziri wa Mambo ya nje wa mataifa hayo wakijadili usambazaji wa chanjo ya corona ulimwenguni.

Shirika la Afya Duniani WHO lilikuwa limehimiza mataifa yalioendelea kusaidia nchi masikini kupata chanjo hizo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles