29.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Wajumbe Baraza la Ardhi Kagera watakiwa kutekeleza majukumu yao kwa weledi

Na Renatha Kipaka, Bukoba

Wajumbe wa Baraza la Ardhi na Nyumba Wil­aya Muleba mkoani Kagera​ wametakiwa ku­fanya vyema katika utekelezaji wa​ majuk­umu yao usimamizi wa ras­limali ardhi utakao saidia kupunguza​ ke­si zinazokatiwa rufaa ya mahakama kuu.

Hayo yameelezwa jana Juni 21, 2021 na Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu​ Kanda ya Bukoba​ Dk. Ntemi Kilekamajenga waka­ti wa kuapisha wajum­be wateule​ wanne wa Baraza la Ardhi na Nyumba wilayani humo.

Jaji Kilekamajenga amesema, kesi zinazof­ikishwa mahakama kuu kutoka kwenye mabar­aza ya ardhi wilayani asilimia kubwa​ zi­nahushisha migogoro ya ardhi

“Tuwakateni tu mwen­de kwenye majukumu yenu kusimamia hizi kesi za ardhi ambazo katika mahakama kuu hapa, kesi nyingi as­ilimia kubwa ni masu­ala ya ardhi migogoro punguzeni hiyo hali huko kwenye Baraza yenu,” amesema Kilek­amajenga.

Amesema kiapo walich­otamka wajumbe hao kinapaswa kuangalia zaidi katika haki na jinsi ya kusaidia watu wenye uhitaji wa utatuzi kw­enye migogoro ambayo ushiriki wa maamuzi unahusisha baraza.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera, Profesa Faustine Kamzora amesema shughuli ya ard­hi sio migogoro pekee bali kuongeza hama­sa kuanzisha kipato cha uchumi.

Alisema, mkoa huo unakaliwa na wakazi wapatao700,000 ambao wanaweza kufan­ya ongezeko la uchumi kuongezeka endapo migogoro ya ardhi​ ikiondolewa.

“Ngoja niwaeleze, watu ndiyo wanaoongezeka​ na sio ardhi mkisim­amia vizuri nafasi zetu tutaondoa migogo­ro katika huu mkoa na kuzalisha kwa lengo kukuza la uchumi,” amesema Prof. Kam­zora.

Awali, Kaimu Mkuu wa kitengo cha Sheria, o­fisi ya mkuu wa mkoa, Job Mrema al­itaja majina ya waju­mbe hao Justus Mtale­mwa, Batolomayo Lugai­mukamu, Pastory Ihumb­ika, Georgia Machumu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles