27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

WAIRAKI 10,000 KURUDISHWA KWAO

BERLIN, UJERUMANI


WAZIRI wa Maendeleo wa Ujerumani, Gerd Muller, amesema nchi yake na Irak zitashirikiana kutekeleza zoezi la kuwarudisha nyumbani wakimbizi 10,000 wa Irak.

Muller amesema Ujerumani na Iraq zimekubaliana kushirikiana kwa undani zaidi ili kuwasaidia kurudi nyumbani Wairaki hao waliokuwa wameomba hifadhi ya ukimbizi nchini Ujerumani.

Muller aliyekuwa ziara Irak, pia amesema Ujerumani na Irak zitafanya kazi kwa pamoja ili kuwapa fursa za elimu na ajira Wairaki wanaorejea kwao.

Kati ya Wairaki 240,000 wanaoishi nchini Ujerumani kwa sasa, 12,000 miongoni mwao hawajafanikiwa kupata hifadhi ya ukimbizi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles