29.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Wafanyakazi uchukuzi waonywa kuepuka rushwa

Na Sheila Katikula, Mwanza

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Dk Leonard Chamuriho amewataka  wafanyakazi wa sekta ya Uchukuzi kujiepusha na vitendo vya rushwa ili waweze kufanya kazi kwa wajibu na weledi kwa kushirikiana.

Hayo aliyasema jana  wakati akifungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Sekta hiyo jiini  hapa  wenye lengo la kujadili utekelezaji wa majukumu yao ya kazi, utawala na wajibu wa wafanyakazi.

Alisema kuna aina nyingi za  kuomba rushwa  kwa mfano  kuomba zawadi , fedha, mapenzi na kuwanyima watu haki, unyanyasaji wa kijinsia na ukiukwaji wa haki za binadamu kufanya hivyo ni kosa na ikibainika sheria zitachukuliwa.

Alisema ni vema kila mtu kukemea, kujiepusha, kupinga   vitendo vya rushwa kwani ni adui wa haki   siyo vizuri watendaji wabovu na walioshindikana kuonewa  aibu.

“Kila mmoja wenu kuwa mshiriki mkubwa wa kupambana na rushwa  kwani bado kuna  viashiria vya vitendo hivyo  katika maeneo yenu  kwani hatutavumilia  pindi tutakapi baini kuna watu wanafanya,” alisema Chamuriho.

Alipongeza kuwa mtumishi anawajibu wa kufanya kazi kwa weledi kwa  kushirikiana ili kuongeza tija katika utekelezaji wa majukumu ya sekta hiyo siyo kufanya kwa mazoea.

Alisema hawatasita kuchukua hatua pale watakapobaini mazoea yanawekwa mbele badala ya weledi katika utendaji wa kazi.

Aliongeza kuwa ni lazima wajibu uambatane na uelewa wa majukumu ya kila mmoja  pamoja na uhusiano mwema kazini Kati ya viongozi na wafanyakazi.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Mkuu wa sekta hiyo, Gabriel Migire alisema  katika mpango wa watatu unaoendelea kuandaliwa wa maendeleo ya taifa  sekita hiyo imepewa dhamana ya kutekeleza miradi ya kielelezo ikiwemo ujenzi wa reli ya Kati, uboreshwaji wa bandari ya Dar es Salaam na uimarishaji wa kampuni ya ndege Tanzania.

Alisema utekelezaji wa miradi hiyo unasimamiwa na wajumbe  wa sekta hiyo hivyo amewaasa wajumbe hao kutekeleza miradi hiyo kwa ubora unaotakiwa na kulinda thamani ya fedha iliyowekezwa.

Naye Mjumbe kutoka Sekta ya Uchukuzi, Stella Katondo alisema  atahakikisha wanafanya kazi kwa weledi na bidii ili waweze kukamilisha miradi iliyopo kwenye sekta hiyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles