27.1 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Wafanyabiashara wapewa somo kumudu soko la nje

Na Clara Matimo, Mwanza

Ili kuhakikisha wafanyabiashara wa ndani wanapata fursa ya kupeleka bidhaa zao kwenye masoko ya nje ya nchi wamepewa mafunzo  yatakayowasaidia kufahamu vikwazo visivyo vya kikodi waweze kuyafikia masoko hayo kwa urahisi.

TUNASIKILIZA: Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya namna ya kutatua vikwazo kwa biashara visivyokuwa vya kikodi wakimsikiliza mkufunzi wao(hayupo pichani).

Mafunzo hayo ya siku tatu yaliyoanza Mei 9 hadi 11, mwaka huu  yanatolewa jijini hapa  na Kituo cha Biashara za Kimataifa (ITC) kupitia Mradi wa Kuwajengea uwezo  Wajasiriamali katika kuongeza thamani na kupata masoko ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Soko la Ulaya, (Markup).

Akizungumza na Mtanzania Digital, Mratibu wa mradi huo, Safari Fungo, amesema mafunzo hayo ni matokeo ya utafiti walioufanya wa  kuangaliani namna gani taratibu ambazo sio za kikodi  zinaleta changamoto kwenye biashara hapa nchini na kubaini mambo mbalimbali ikiwemo vikwazo na fursa  kwa wafanyabiashara kuingiza bidhaa ndani ya nchi au kwenda nje ya nchi.

“Katika tafiti hiyo tulibaini mambo mengi sana moja ya mambo ambayo yalionekena ni changamoto ya vifungashio, uwezo wa wafanyabiashara kukidhi mahitaji ya soko hasa katika maeneo ya ubora na viwango.

“Utafiti huo tuliufanya miaka miwili iliyopita kwa kushirikiana na serikali kupiti Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara  tuliuzindua Aprili 14, mwaka huu baada ya kuuzindua tuliona ni busara yale yaliyopatikana kwenye tafiti yaweze  kushuka chini kwa watanzania, tunakwenda sehemu mbalimbali hapa nchini tumeanza na mikoa ya kanda ya ziwa,” alisema Fungo na kuongeza.

Malengo yetu ni mawili, kuwajengea uwezo wadau katika masuala ya biashara kutoka sekta za uma na binafsi kwenye masuala ya kibiashara waweze kupata mbinu ya kujua masoko, mahitaji ya masoko ni yapi(market access) ili  wafanyabiashara watumie taarifa hizo kwa wafanyakazi wa serikali wawasaidie jumuiya ya wafanyabiashara  waweze kufanya biashara vizuri na kuhakikisha yale majibu ya kwenye tafiti yanawafikia wadau mbalimbali,”alisema.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo  akiwemo Leopord Lema na Bakari Kadabi, walisema wanakumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo kupeleka bidhaa zao sokoni  nje ya nchi bila kuwa na taarifa za kutosha hivyo wamepata fursa ya  kujua kwa uhakika vitu vinavyohitajika pamoja na gharama  zisizo za kikodi.

 “Miongoni mwa changamoto tulizonazo ni kukosa taarifa, hatuna kabisa taarifa  ya kujua misingi ya biashara inaendaje kidunia hivyo mafunzo haya yatatusaidia exporters na importers kurahisisha jinsi ya kufanya biashara baina ya nchi yetu na nyingine,”alisema Kadabi ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Wavuvi Tanzania, (Tafu).

Mkufunzi wa mafunzo hayo Mwalimu Mwandamizi kutoka Chuo kikuu cha Dar es Salaam, Dk.Petro Magai, alisema mafunzo hayo yatatoa fursa kwa wafanyabiashara kuongeza uelewa kuhusu masoko.

Meneja wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo Vidogo(Sido),  Mkoa wa Mwanza, Bakari Songwe, alisema:

“Sisi sido kama wadau muhimu katika utoaji wa mafunzo mbalimbali  kwa wajasiriamali tutasambaza elimu hii kwa wajasiriamali wetu waweze kunufaika na kupata  taarifa mbalimbali zinazohusu biashara ya kimataifa,”.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles