24.4 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Wachumi waonya uchumi wa Marekani kuporomoka karibuni

WASHINGTON, MAREKANI

NUSU ya wataalamu wote wa uchumi nchini hapa wanasema wanadhani uchumi wa taifa hilo utatumbukia katika mporomoko kufikia mwishoni mwa mwaka ujao.

Baadhi ya wanauchumi wanakadiria kwamba mtikisiko mkubwa wa kiuchumi utaanzia mwishoni mwa mwaka 2021.

Utafiti huo umetokana na uchunguzi uliofanyika karibuni na Chama cha Taifa cha Wanauchumi na Wafanyabiashara nchini Marekani (NABE).

Asilimia 10 tu ya wanauchumi hao wamekadiria kuwa mtikisiko wa uchumi utaanza katika kipindi hiki cha mwanzo wa mwaka huu.

Asilimia 11 ya wanauchumi wanatarajia kwamba mporomoko wa kiuchumi utaepukika mwaka 2021.

NABE ndiyo wenye dhamana ya kuhakiki usimamizi wa viwango vya riba vya hazina kuu ya Marekani.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles