26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

WABUNGE WADAI MAZINGIRA YA NDANI HAYAJABORESHWA KWA WAFUGAJI

Maregesi Paul, Dodoma

Mbunge wa Monduli, Julius Kalanga (Chadema), amesema wafugaji wataendelea kutorosha mifugo na kuiuza nje ya nchi kwa kuwa mazingira ya ndani hayajaboreshwa kwa wafugaji.

Aidha, mbunge huyo ameitaka serikali kufuta tozo na kodi zilizoko katika sekta ya ufugaji kama ambavyo imekuwa ikifuta kodi na tozo hizo katika sekta ya kilimo.

Kalanga ameyasema hayo bungeni leo Mei 17, alipokuwa akichangia bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2018/19 iliyowasilishwa na Waziri wa Wizara hiyo Luhaga Mpina.

Kwa upande wake Mbunge wa Viti Maalumu, Suzan Masele (Chadema), amelalamikia operesheni inayofanywa kwa ajili ya kudhibiti uvuvi haramu katika Ziwa Victoria.

“Operesheni hiyo imejaa kasoro nyingi kwa kuwa wavuvi wananyanyaswa ikiwa ni pamoja na kupigwa na kutozwa faini kubwa zisizoendana na sheria za nchi,” amesema.

Hoja ya mbunge huyo iliungwa mkono na Mbunge wa Viti Maalumu, Agnes Marwa (CCM), aliyelalamikia operesheni hiyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles