25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Vita ya kibabe wachezaji wa kikapu Bongo

Sharifa Mmasi, Mtanzania Digital

LIGI ya mpira wa Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (RBA), inaendelea Ijumaa hii ambapo, mchezaji Hajji Mbegu anayeitumikia klabu ya Ukonga Kings wiki hii ndiye anayeshika nafasi ya kwanza akifanikiwa kuifungia timu yake jumla ya pointi 140 ambazo, hazijafikiwa na wapinzani wengine.

Mchezaji anayeshikilia nafasi ya pili ni Enrico Mangela mwenye jumla ya pointi 121 akifuatiwa na Leek Deng wa Ukonga Kings kwa alama 113 akiwa nafasi ya tatu.

Kwa upande wa wanawake, mchezaji Jesca Ngisaise wa JKT Stars anashika nafasi ya kwanza akiifungia klabu yake jumla ya alama 145 huku Monalisa Kaijage wa Ukonga Queens akikamata namba mbili kwa umiliki wa pointi 80 wakati Nyanjura Masinde akisalia nafasi ya tatu kwa alama 76.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles