26.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

VIONGOZI CHADEMA KULA PASAKA MAHABUSU

Na Kulwa Mzee, Dar es Salaam

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeamuru viongozi wa sita wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), akiwamo Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe kuletwa mahakamani hapo Jumanne Machi 3, ili kutimiza masharti yanayowataka kuwa na wadhamini wawili watakaosaini Sh milioni 20 kwa maandishi.

Uamuzi huo umetolewa na Hakimu mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri baada ya mabishano makali ya kisheria ambapo Jamhuri wamewasilisha nia ya kukata rufaa kupinga uamuzi wa mahakama kutoa dhamana kwa washtakiwa hao.

Wakili Mkuu wa Serikali, Fatma Nchimbi andiye amewasilisha nia ya kupinga washtakiwa hao kupewa dhamana hoja iliyopingwa na Wakili wa utetezi, Peter Kibatala.

Baada ya mabishano hayo, Hakimu Mashauri alisema: “Hoja ya kukata rufaa kupinga uamuzi wa kuwapa dhamana washtakiwa hao, imewasilishwa mapema na inatoa amri washtakiwa hao waletwe Jumanne ili kutimiza masharti ya dhamana kwa kuwa leo hawapo mahakamani.”

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles