MICHIGAN, MAREKANI
MREMBO anayekuja kwa kasi kwenye Bongo Fleva, Violet Viola ‘Violla’, amewaomba wapenzi wa muziki huo wampe nafasi kwa kusikiliza na kutazama video ya wimbo wake, Tushikane.
Akizungumza na Mtanzania Digital, Violla alisema, Tushikane ni wimbo wake wa kwanza ambapo video imefanyika maeneo ya Grand Rapids, Michigan nchini Marekani huku audio ikitengenezwa na prodyuza Kitonzo.
“Nashukuru mapokezi ni makubwa ya wimbo wangu Tushikane, bado nahitaji sapoti ya mashabiki kwa sababu ndio kwanza nimeanza safari yangu ya muziki, hii ni ngoma yangu ya kwanza ambayo tayari nimeweka video kwenye chaneli yangu ya YouTube,” alisema Violla.