24.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 18, 2024

Contact us: [email protected]

Vijana wenye nguvu waachia ‘EP’ Shusha Roho Wako

Des Moines, Marekani

BENDI ya muziki wa Injili nchini Marekani, Vijana Wenye Nguvu, imeachia albamu yake fupi (EP) inayofahamika kama Shusha Roho Wako inayopatikana duniani kote kwenye mitandao ya kusikiliza na kupakua muziki.

Akizungumza na Mtanzania Digital mmoja ya waimbaji wanounda bendi hiyo, Diedonne amesema Vijana Wenye Nguvu wametoa EP hiyo ikiwa na nyimbo nzuri tano zenye mguso wa kipekee kwa yeyote atakayesikiliza.

“Bendi yetu inaundwa na vijana watatu ambao ni Dieudonne, Fidel na M’mewa sasa tumetoa EP yetu mpya inayokwenda kwa jina la Shusha Roho yenye nyimbo nzuri zenye upako kama vile Shusho Roho Wako, Niongoze, Wandi Pasa Malo, Nasema Asante na Mwite Yesu ambayo sasa inapatikana kwenye platforms zote za muziki,” amesema Dieudonne.

Aidha, aliongezwa kwa kuwaomba wapenzi wa muziki huo wawatafute kwenye mitandao ya kijamii ya Facebook, Instagram na YouTube kwa jina la Vijana Wenye Nguvu huku wakiishuskuru studio ya Heaven Music Studio chini ya prodyuza Pasa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles