24.4 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Vazi la Niqab lapigwa marufuku Rwanda

Vazi la Niqab
Vazi la Niqab

KIGALI, RWANDA

JUMUIYA ya Waislamu nchini Rwanda imepiga marufuku wanawake nchini humo kuvaa vazi la nigab linalofunika mwili mzima.

Ilisema hatua hiyo ya kupiga marufuku vazi hilo linalovaliwa na wanawake ni kutokana na sababu za kiusalama kwa Waislamu na Wanyarwanda kwa ujumla.

Hatua hiyo inakuja baada ya kundi la Waislamu zaidi ya 17 kushikiliwa na kufunguliwa mashtaka kwa kusajili vijana wa kujiunga na kundi lijiitalo Dola la Kiislamu (IS).

“Hili vazi ni la Kiislamu, hata hivyo limeanza kutumika vibaya kwa madhumuni ya kudhuru usalama wa Waislamu na vitendo vinavyokinzana na mafunzo ya dini ya Kiislamu,” taarifa ilisema.

“Jambo la pili ni usalama wa nchi. kwa sababu watu wanajificha na kutenda vitendo pasi na kutaka kuonekana.

“Tumeona fikira potofu tayari ikishamiri na ndipo tukachukua uamuzi huu wa kuzuia kuenea kwa uovu,” alisema Sheikh Mussa Sindayigaya.

Katika Msikiti Mkuu wa Nyamirambo jijini Kigali, Waislamu wengi wanaonekana wakiingia msikitini, lakini hakuna hata mmoja aliyevaa vazi hilo miongoni mwa wanawake au mabinti wanaoingia humo.

Wanaounga mkono uamuzi wa jumuiya hiyo wanasema kuwa Niqab ilikuwa imeanza kutumika kuficha maovu mengi katika jamii.

Aidha wanasema wanawake Waislamu wanapaswa kuwajibika kwa kujiepusha na maovu ambayo sasa yameanza kuchipuka kwa kisingizio cha Niqab.

Hata hivyo wapo baadhi ya Waislamu waliokasirishwa na uamuzi huo, lakini hawakutaka kuzungumzia suala hilo wakisema kuwa wanahofia usalama wao.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles