31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

UTURUKI YAITISHA MKUTANO KUJADILI MASHAMBULIZI YA MSIKITI NEW ZEALAND

Uturuki imeitisha mkutano wa dharura na Shirika la Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) kujadili mashambulizi ya msikiti wa New Zealand na “kuongeza vurugu kwa misingi ya Uislamu”.

Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi hiyo imesema katika taarifa yake kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Mevlut Cavusoglu ndiye atakuwa Mwenyekiti wa mkutano huo utakaofanyika mjini Istanbul siku ya Ijumaa.

“Uturuki, kama Mwenyekiti wa Mkutano wa OIC, imepanga kufanya mkutano huo wa dharura ili kujadili vurugu inayoongezeka kutokana na Uislamu, ubaguzi wa rangi na unyanyasaji wa ubaguzi, hususan mashambulizi ya kigaidi yaliyolenga misikiti miwili huko New Zealand mnamo 15 Machi 2019.

Pia taarifa imesema kuwa mbali na wanachama wa OIC, wawakilishi wa Umoja wa Mataifa, Umoja wa Ulaya na Shirika la Usalama na Ushirikiano katika Ulaya (OSCE) pia wamealikwa kwenye mkutano huo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles