27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

UTURUKI, URUSI, IRANI ZAJIPANGA  KUVUNJA NGUVU YA DOLA YA MAREKANI

 

NKARA,Uturuki


RAIS wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, amesema nchi yake itaendelea kushirikiana kibiashara na  nchi washirika wake kwa kutumia sarafu  moja ikiwamo Urusi, ili kukabiliana na nguvu ya Dola ya Marekani.

Kiongozi huyo aliyasema hayo juzi wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika mji wa  Rize akisema Uturuki imeamua kufanya hivyo ili kuendeleza uhusiano kibiashara na mataifa hayo ambayo ni washirika wake.

Alisema, katika mkakati huo atashirikiana na nchi za Urusi, China, Iran na Ukraine ili waweze kupanua wigo wa kibiashara na kasema kuwa na kama mataifa ya Ulaya yatang’ang’ania matumizi  ya dola watakuwa wameshajipanga kukabiliana na suala hilo.

“Tunajiunga kibiashara katika sarafu moja ya mataifa  ya  China, Urusi, Iran, Ukraine, ambayo ina fursa kubwa zaidi ya biashara baina ya nchi hizi.Kama nchi za Ulaya zinataka kuondokana na shinikizo la dola, tuko tayari kujenga mfumo sawa na wao ,” alisema.

Katika hotuba hiyo Rais Erdogan alibainisha kuwa Serikali yake ya Ankara haiwezi  kuvumilia hali ngumu ya vikwazo vya  kiuchumi vilitangazwa dhidi ya dunia nzima na mashinikizo wanayowekewa nchi nyingine, ambazo zinatishiwa na vikwazo.

Alitamba akisema kwamba hakuna wanasiasa au nchi yoyote duniani kote ambayo itafanikiwa kwa  kufuata sera ya uadui zinazoelekezwa dhidi ya Uturuki.

Awali msemaji wa Rais huyo, Ibrahim Kalin, hivi karibuni alieleza katika mahojiano na Gazeti la Daily Sabah kwamba Marekani ina hatari ya kupoteza Uturuki kama mshirika wake.

Gazeti jingine la New York Times lilichapisha makala ya  Rais Erdogan, akieleza kuwa  vitendo vya Marekani inavyovifanya  dhidi ya nchi hii ndivyo vilivyochangia serikali yake  kutafuta washirika wapya.

Uhusiano baina ya mataifa haya mawili, ulianza kuzorota, baada ya Rais  Donald Trump wa Marekani, kuongeza ushuru kwa bidhaa alminium  na chuma kwa asilimia  20 hadi  50 zinazotoka nchini hapa.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles