Viwango vya afya ya maungo ya watoto milioni 1.1 walio kati ya umri wa miaka tisa hadi 17 kutoka mataifa 50 vilifanyiwa ukaguzi.
Watoto hao walifanyiwa zoezi la kukimbia umbali wa mita 20, ili kukagua afya za maungo yao.
Grant Tomkinson, mmoja ya watafiti wakuu wa chuo cha Kusini mwa Australia ameeleza kuwa watoto wa Tanzania waliibuka washindi kutokana na utendaji wao. (Source BBC)