26.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Urusi, Israel kuijadili Syria

 TEL AVIV,Israel

WAZIRI Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amesema maofisa wa jeshi la hapa na Urusi watakutana siku chache zijazo mjini Moscow kwa ajili ya kujadili hali ilivyo nchini Syria.

Waziri Mkuu huyo aliyasema hayo jana katika  mkutano wake na viongozi wa serikali na akasema kwamba tayari alishazungumza na Rais wa Urusi, Vladimir Putin

“Jana (juzi) nilizungumza na Rais wa Urusi Vladimir Putin. Tulikubalina  kwamba wajumbe wetu wa kijeshi ambao wanashirikiana nchini  Syria wakutane kwa haraka iwezekavyo na suala hili nadhani litafanyika siku chache zijazo na pia nina matumaini watakutana mjini Moscow,”alisema waziri mkuu huyo.

Idara ya Habari ya Ikulu ya Urusi  ilieleza kuwa Rais Putin na  Waziri Mkuu Netanyahu  walifanya mazungumzo kwa njia ya simu juzi na kisha wakakubaliana kukutana hana kwa hana baadae.

“Kupitia mawasiliano hayo ya simu viongozi tumekubaliana kukutana mjini Paris, ili kuhakikishiana kuzidi kushirikiana  kati ya majeshi ya Urusi na Israel  tuliouanzisha kwa  iaka mingi iliyopita,”alisema Netanyahu .

Viongozi hao pia wamewahi kufanya mazungumzo mjini Paris Novemba 11 mwaka huu wakati wa maadhimisho ya kumbkumbu ya vita Kuu ya Kwanza ya Dunia.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles